Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula akisalimiana na katibu wa Jumuiya ya Watanzania Columbus, Ohio Bi. Happiness Salukele wakiwemo wajumbe wa Jumuiya Nasra Murumah, Chiseko Hamisi na kushoto ni mweka hazina wa Jumuiya Bi. Vera Teri
 Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Mumewe Bwn. George Mulamula wakikaribishwa kwenye mgahawa wa Mitchell's Steakhouse wa Columbus, Ohio na wajumbe wa Jumuiya wakiwemo viongozi kwenye chakula cha jioni walichomuandalia Mhe. Balozi na Mumewe. Mhe. Balozi Liberata Mulamula yupo Columbus kwa ajili ya Fundraisng ya Jumuiya ya Watanzania Columbus, Ohio itayaofanyika leo Jumamosi April 19, 2014 katika ukumbi wa Comfort Inn uliopo 1213 E. Dublin Granville Road, Columbus, Ohio na kiingilio ni $15 na muziki utaporomoshwa na Dj Luke kutoka DC.
 Wajumbe wakimpokea Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Mumewe Bwn. George Mulamula mara tu walipowasili kwenye mgahawa wa Mitchell's Steakhouse, anayesalimia na Balozi ni mjumbe Michael Mngodo.
Kutoka kushoto ni katibu wa Jumuiya Bi. Happiness Salukele, Mume wa Balozi Bwn. George Mulamula, Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula, mweka hazina Bi. Vera Teri na mjumbe Nasra Murumah.
 Wajumbe wakiangalia menu tayari kwa kuagiza chakula cha jioni walichomuandalia Mhe. Balozi pamoja na Mumewe.
 Wajumbe wakiwemo kwenye chakula cha jioni walichomuandalia Balozi pamoja na mumewe.
 Kutoka kushoto ni Deo Mwalujuwa, mjumbe Joe Ngwilizi, mjumbe Michael Mngodo na mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Columbus Ohio, Bwn Jimmy James.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...