Wasamalia
wema wakijaribu kulinasua gari aina ya Toyota Corolla (namba zake za
usajili hazikuweza fahamamika mara moja kutokana na kutokuwepo)
lililoingia kwenye mtaro baada ya dereva wake kuzidiwa maarifa ya
kiudereza na kujikuta akiingia mtaroni,katika eneo la Mafiat mkabala na
kituo cha mafuta cha Oilcom jijini Mbeya asubuhi hii.Dereva wa Gari hilo
pamoja na mtu mwingine mmoja wamejeruhiwa na kukimbizwa hospital kwa
matibabu.Chanzo cha ajali hiyo inaelezwa ni mwendo kasi aliokuwa nao
Dereva wa gari hilo.
Wasamalia wema hao wakiangalia namna ya kuweza kulichomoa gari hilo.
Hayaaaa..... Moja.... mbili.... tatuuu twendeeeeeeee......
Mara wakafanikiwa kulitoma kwenye mtaro huo.Picha na Fadhil Atick,Mbeya
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...