wasanii wa bendi ya fm Academia wakiwa jukwaani wanaimba wapili kulia ni Rais wa bendi Nyoshi
Rapa wa bendi  ya Fm Academia akiwa anashambulia jukwaa wakati wa shoo.
wanenguaji wa bendi ya Fm wakiwa kazini  wote hawa watakuwepo katika  uzinduzi huu wa Albamu ya Chuki ya nini usikose ni balaa
Fm  Academia baada ya kukaa kwa muda wa miaka 4 (minne) yaani kuanzia mwaka 2010 mpaka 2013 sasa wanatarajia kuzindua rasmi  album mpya kabisa inayojulikana kwa jina la Chuki ya nini ndani ya jiji la Arusha na vitongoji vyake .

 Album ya chuki ya nini imebeba nyimbo kumi ndani yake,nazo ni:-Chuki ya nini, Fataki ,Otilia ,Ndoa ya kisasa,Neema,Dai chako ulaumiwe,Maisha,Madudu,Miraessa.album ya chuki ya nini ni album yenye kiwango cha kimataifa ambapo nyimbo hizi zote zitazinduliwa rasmi septembar tano mwaka huu ndani ya viwanja vya  ukumbi wa Triple A jijini Arusha

Akizungumza na waandishi  wa habari jijini hapa mkurugenzi wa SB Intamenti Seif Manyota alisema kuwa bendi hiyo inatarajia kutua jijini Arusha kwa kishindo kwa ajili ya uzinduzi huu wa albamu mpya ambapo alibainisha kua tukio hilo litakuwa la kihistoria.

Alisema kuwa  hii ni mara ya kwanza kwa bendi hii  kuzindua albamu  nje ya mkoa wa dar es salaam na kwa hivyo wameamua kuwapa heshima kubwa wapenzi wa bendi hiyo wa mkoa wa Arusha  pamoja na mikoa ya kanda ya kaskazini kwa ujumla hii ikiwa ni heshima ya kipekee.

"uzinduzi huu wa  albamu sio tu tunazindua  nyimbo mpya bali tunazindua pia vyombo vipya na staili mpya za kuicheza gwasuma kama vile mnavyojua bendi ya fm  ni wazee wa pamba wazee wa kushambulia jukwaa"alisema Manyota

Aidha alibainisha kuwa kwa mkoa wa Arusha wameamua kuwapa kipaumbele na pia kwakuwa kunawapenzi wengi wa ngwasuma wameamua kufanya shoo hii nje ambapo ,kutafugwa jukwaa la kisasa  kabisa.

Alitaja baadhi ya nyimbo ambazo zipo katika albamu ambayo inazinduliwa kuwa ni pamoja na Chuki ya nini,ndoa ya kisasa fataki  pamoja na nyinginezo.

Aidha kwa upande  mungine alisema uzinduzi huu autaishia Arusha tu bali wakazi wa Moshi na Tanga nao watapata burudani hii na kuzitambua staili mpya pamoja na nyimbo mpya zilizopo kwenye albamu hii.

Alisema kua pia kutakuwa na CD na DVD za albamu hiyo mpya iliyozinduliwa huku akisema kuwa kwa upande wa Arusha kiingili    akuwa 20000 na unapatiwa CD moja buru mlangoni.

kwa upande wa Rais wa bendi hiyo Nyoshi alisema kuwa timu  yake yote imejipanga vyema kuwapa burudani ya nguvu wakazi wa Arusha  na kuwapa staili mpya ikiwemo ile ya vundesa  ambapo alisema kuwa wameiboresha na imekuwa ya kiufasaha  zaidi  na ina vinjonjo vingi zaidi ,staili tamu  pamoja na maneno matamu.
Alisema kuwa lengola kubwa la kuzindua albaimu hii apa jijini Arusha ni pamoja na kuwaelewesha wapenzi wao nyimbo mpya na kuakikisha wapenzi wao wanajua staili zao zote za  nyimbo hizo na  sio ivyo tu pia alisema kuwa kwa kipindi  hiki wanataka kuwa wakazi wa arusha zawadi ya kuwaletea wasanii wote wa bendi hiyo ambapo alisema wapo 32  na wote watafika jijini Arusha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...