Wafanyakazi wa Benki ya Exim tawi la Mwanza na wawakilishi wa
gereza la Butimba wakiwa katika picha ya pamoja, muda mfupi baada ya Benki hiyo
kukabidhi vifaa vya usafi kwa gereza la
Butimba lililopo jijini Mwanza hivi karibuni. Mchango huo ni sehemu ya shughuli
za kibenki za kijamii lakini pia ukilenga kusaidia wafungwa kubadili tabia.
Exim
Bank imeahidi kuendelea kusaidia juhudi za serikali katika kuboresha
hali ya magereza nchini, ikiwa ni sehemu ya shughuli zake za kibenki za
kijamii. Benki iyo imekabidhi vifaa vya usafi kwa wanawake wanaotumikia
vifungo
katika gereza la Butimba jijini Mwanza, hatua inayolenga kuwasaidia na
kuwaelimisha
wanawake hao kubadili tabia.
Akizungumza katika hafla fupi iliyofanyika katika gereza la Butimba
jijini Mwanza hapo jana, Mkuu wa Matawi wa Benki ya Exim Mwanza, Bw. Justus Mukuras alisema mchango huo utawasaidia kwa
kiasi kikubwa wafungwa walio katika gereza hilo. Alisema mbali na mchango wa vifaa hivyo, benki hiyo iliajiri
mwanasaikolojia ambaye alizungumza na wanawake hao na kuwapa faraja pamoja na
kuwafundisha mbinu mbalimbali za maisha. Lengo likiwa kuwafanya kuwa mfano bora
katika jamii zao pindi watakaporudi uraiani.
“Hii ni sehemu ya shughuli
zetu za kijamii na hatulengi kuishia hapa, hizi ni jitihada endelevu zilizo
chini ya kampeni ya benki yetu ya kusaidia wafungwa wa kike nchini. “Pamoja na mambo mengine, kampeni hiyo inalenga kuwafundisha
wafungwa mbinu mbalimbali za maisha na kuwafanya wawe watu bora zaidi. Tutaendelea
kuwasaidia vifaa vya usafi pamoja na vifaa vingine kwa watoto wanaoishi na mama
zao katika magereza,” alisema Bw. Mukuras.
Wafungwa wengi nchini wanakabiliwa na uhaba wa vifaa vya usafi
pamoja na vyakula; hii inatokana na idadi kubwa ya wafungwa katika magereza
hali inayopelekea mlipuko wa magonjwa.
“Sisi kama benki tungependa
kutekeleza jukumu letu la kusaidia jamii hususani wanawake wanaotumikia vifungo
katika magereza pamoja na watoto wanaoishi na mama zao katika magereza hayo
kwani baadhi yao wanakabiliwa na upungufu wa virutubisho na afya duni. Ukipata
nafasi ya kuingia katika magereza ndipo utakapobaini idadi ya matatizo wanayokumbana
nayo,” aliongeza Bw. Mukuras.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...