Na Woinde Shizza,Arusha.

Kiongozi wa  matukio ya ulipuaji wa mabomu na umwagiaji tindikali viongozi wa dini aliyejulikana kwa jina la Yahaya Hassani Omary ameuwawa na jeshi la polisi wakati alivyokuwa akijaribu kukimbia.

Akithitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoani Arusha,SACP Liberatus Sabas (pichani) Alisema kuwa tukio hilo limetokea  October 19 majira ya saa tano na nusu  katika barabara ya babati mkoani Arusha wakati alipokuwa akijaribu kuwakimbia polisi.

Alisema kuwa mtuhumiwa huyo wa ugaidi alishikiliwa wiki mbili zilizopita  huko mkoani Morogoro  mara baada ya kutafutwa kwa muda mrefu na hapo jana alikuwa akipelekwa wilayani kondoa mkoani Dodoma  kwa ajili ya kwenda kuonyesha sehemu ambazo alikuwa ameficha mabomu mengine.

"mtuhumiwa huyo alikuwa anasakwa kwa muda mrefu bila mafanikio kwani alikuwa hakai sehemu moja ila jeshi la polisi huko mkoani morogoro lilimkamata wiki mbili zilizopita na baada ya kufanyiwa mahojiano alisema ameficha mabomu mengine huko kondoa na jana alikuwa akipelekwa kuonyesha ndipo alipotumia trikizake ambazo amefundishwa za ugaidi kwa kupiga judo na kutaka kuwakimbia askari ndipo akapigwa risasi mbili"alisema Sabas

Alitoa wito kwa wananchi kuendelea kuwafichua waovu  ili kuwaza kuteketeza matukio ya uhalifu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Alikua analipwa mshahara na nani huyo gaidi. ?

    ReplyDelete
  2. Mtuhumiwa alikuwa anasafirishwa kwenye mkokoteni mpaka akaruka na kuanza kukimbia? Je, hakufungwa pingu ndg. Kamanda? Just curious.

    ReplyDelete
  3. Jamani ni hakika ni yeye?! Je alishataja wengine?

    ReplyDelete
  4. Hii ni kama execution ya kukusudia. Huyo ni mshukiwa tu na hajakutwa na hatia na mahakama yeyote. Kumuua mshukiwa asiyekuwa na silaha ni kosa kubwa sana. Hata kama ametaka kukiumbia. Maswali polisi wanatakiwa kujibu ni kuwa; Je mshukiwa wa kosa kubwa kama hilo la ugaidi akasafirishwe bila pingu miguuni au mikononi kiasi kwamba ameweza kuwapiga polisi judo? Sio amepewa mwanya akimbie ili apigwe risasi afe. Human Rights Group fanyeni Uchunguzi huru. Alexbura Dar

    ReplyDelete
    Replies
    1. Una upeo mkubwa sana mkuu. Ndo tanzania yetu hii

      Delete
  5. well done!!

    ReplyDelete
  6. well done police tz hayo ndio maneno tunataka kuyasikia, watu kama hawa hawatakiwi kwenye jamii yetu, maliza wote kuwe na amani

    ReplyDelete
  7. Siasa tupu!

    ReplyDelete
  8. What are the use of electroshock weapons?

    ReplyDelete
  9. Aisee tuko nyuma sana kwenye maswala ya law enforcement handling.
    God help us

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...