Wanachama wa Mtandao wa Habari za Kijamii Tanzania (Mhakita), wakifanya usafi katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya tamasha la Ujirani Mwema, wilayani Kilosa mkoani Morogoro, hivi juzi. Picha na Mpigapicha Wetu.
KIASI cha sh milioni 25 hutumika kila mwaka katika hifadhi ya Taifa ya Mikumi iliYopo wilayani
Kilosa mkoani Morogoro kwa ajili ya shughuli za usafi wa mazingira na kuhudumia wanyama
wanaogongwa katika barabara kuu iendayo Iringa na Morogoro inayopita katika hifadhi hiyo.
Kaimu mkuu wa hifadhi hiyo Dattomax Selanyika ,alisema hayo jana wakati akizungumza na
waandishi habari waliotembelea katika hifadhi hiyo na kupata fulsa ya kufanya usafi wa
mazingira kwa lengo la kupinga masuala ya ujangili kupitia mtandao wa habari za kijamii
Tanzania MHAKITA.
Alisema kati ya fedha hizo milioni 12.5 hutumika kwaajili ya uokotaji wa takataka zinazotupwa na
wasafiri wanaotumia barabara hiyo.
‘’ Usafi huo hufanywa na vibarua kuanzia eneo la Doma hadi Mikumi umbali wa kilomita 50, na
shughuli hiyo hufanywa mara tatu kwa wiki’’ alisema Selanyika.
Aidha alisema katika maeneo yaliowekwa matuta ili magari yaweze kupunguza mwendo
kutokana na kuwa ni vivuko vya wanyama pamegeuzwa ndio sehemu ya kutupa takataka kwa
wasafiri hao.
Alisema utupaji wa takataka katika hifadhi hiyo una madhara makubwa kwa wanyama kwani
baadhi ya takataka husababisha wanyama kupoteza maisha wakizila.
Hata hivyo alisema kumekuwa na tabia ya baadhi ya madereva kwenda mwenzo kasi katika
hifadhi, hiyo kinyume na sheria na kwamba kusababisha kuwagonga wanyama.
Kwa upande wake mkuu wa idara ya ikologia wa hifadhi hiyo Crispin mwinuka alisema idadi ya
wanyama wanaogongwa katika hifadhi hiyo wamekuwa wakiongezeka mwaka hadi mwaka
ambapo katika kipindi cha miaka 2009 hadi 2013 jumla ya wanyama 604 waligongwa katika
barabara hiyo na kupoteza maisha.
Alisema mwaka 2012 wanyama waliogongwa walikuwa 111 huku mwaka 2014 walikuwa 132.
Pia alisema katika kipindi hicho hicho jumla ya kilogramu 21,907.80 zilitupwa katika hifadhi hiyo
na kusababisha hifadhi hiyo kuingia hasara kubwa katika kuokota taka hizo.
Aliwataka wasafiri wanaotumia barabara hiyo kujenga tabia ya kuweka vifaa vya kuhifadhia
takataka katika vyombo vya usafiri ili kuepusha tatizo hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...