Serikali ya Zambia imetangaza kuwa mazishi ya Rais Michael Chilufya Sata (pichani) yatafanyika siku ya Jumanne tarehe 11 Novemba 2014, katika eneo la makaburi lililotengwa rasmi kwa ajili ya kuzikwa Marais linaloitwa Embassy Park, Lusaka, Zambia.Mwili wa Rais Sata unategemewa kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kenneth Kaunda, Lusaka, siku ya Jumamosi tarehe 1 Novemba 2014. Mara baada ya mwili kupokelewa utapelekwa katika Ukumbi wa Mkutano wa Kimataifa wa Mulungushi ambapo watu wote watapata fursa ya kuuaga. Dkt. Guy Scott, Makamu wa Rais ataweka shada la maua.Taratibu za kuaga mwili wa Rais Sata zitafanyika katika Ukumbi wa Mulungushi zitaanza rasmi siku ya Jumapili tarehe 2 hadi Jumapili tarehe 9 Novemba 2014. Misa ya kuaga itafanyika siku ya Jumannne, tarehe 11 Novemba 2014 katika viwanja vya mashujaa, Lusaka. na baada ya hapo mwili utapelekwa Embassy Park kwa mazishi.MUNGU AMLAZE MAHALI PEMA PEPONI, AMINAUBALOZI WA TANZANIA, LUSAKA
Home
Unlabelled
RAIS SATA WA ZAMBIA KUZIKWA NOVEMBA 11, 2014 JIJINI LUSAKA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...