Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias
Chikawe (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo mabati 2000
kwa ajili ya ujenzi wa Maabara za Shule 20 za Sekondari wilayani humo. Waziri Chikawe
ametoa msaada huo baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa agizo kwa kila mwana jamii nchini
kuchangia ujenzi wa maabara katika shule za Kata nchini.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias
Chikawe (wapili kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo, Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Wilaya hiyo, Abdalla Chikawe (wapili kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya hiyo, Valery Kwembe wakiyaangalia msaada wa mabati yaliyotolewa na
Mbunge wa Jimbo hilo kwa ajili ya kuzisaidia Shule za Sekondari za Kata kwa ajili ya ujenzi wa
maabara. Makabidhiano ya mabati hayo 2000 yalifanyika nyumbani kwa Waziri Chikawe mjini
Nachingwea leo. Picha zote na Felix Mwagara.
Changamkeni wanasiasa, uchaguzi mwakani!
ReplyDelete