ASILIMIA 61 ya ardhi nchini imeharibika kutokana uharibifu wa
mazingira ya ardhi katika vyanzo vya mbalimbali na kusababisha kuzama
kwa baadhi ya viziwa kutokana na mabadiliko ya tabianchi.
Hayo ameyasema leo jijini Dar es Salaam,Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu
wa Rais-Mazingira,Mhandisi Binith Mahenge wakati akitangaza
maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yatakayofanyika Juni 5 mwaka
huu mkoani Tanga.
Mahenge amesema Juni 5 ya kila mwaka iliamuliwa na Umoja wa Mataifa
mwaka 1972 kuwa Siku ya mazingira duniani kutokana na kuonekana baadhi
ya vyanzo vinapotea kutokana na uchafuzi mazingira.
Amesema mikoa ambayo imekuwa kame kutokana na uharibifu wa mazingira
ni Dodoma,Shinyanga,Geita,Singida,Simiyu na Kilimanjaro huku kasi ya
ukataji miti ikiwa inaongezeka na kufikia hekta 400, 000 kupotea kila
mwaka nchini.
Waziri huyo ameunga mkono kwa Kampuni ya simu za mikononi Airtel
kuungana kuadhimisha siku ya mazingira kwa kuchangia kutoa elimu kwa
njia ujumbe mfupi.
Afisa Mawasiliano na Matukio wa Airtel,Dangio Kaniki,amesema watatoa
ujumbe mfupi kwa ajili ya kutoa elimu kwa katika kuhamasisha utuzaji
wa mazingira na kutaka makampuni mengine yajitokeze kuunga juhudu za
utuzaji wa mazingira.
Dangio,amesema ujumbe mfupi wataotoa katika utuzaji wa mazingira
katika maadhimisho hayo ni zaidi ya Sh.milioni 90 ambazo Airtel
ingepata kutokana na kutuma ujumbe huo.
Afisa Usalama na Mazingira wa Airtel, Mazoya Ncheye (pili kulia) akimkabidhi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Binilith Mahenge msaada wa moja ya fulana zilizotolewa na Airtel Tanzania, kwa ajili ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kitaifa yatafanyika Juni 1-5 mwaka huu, mkoani Tanga, katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel, Dangio Kaniki.
Afisa Usalama na Mazingira wa Airtel, Mazoya Ncheye (kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais Dk. Julius Ningu msaada wa moja ya fulana zilizotolewa na Airtel Tanzania, kwa ajili ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo kitaifa yatafanyika Juni 1-5 mwaka huu, mkoani Tanga, katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Wanaoshuhudia ni Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel, Dangio Kaniki (wa pili kushoto) na (kulia) ni Meneja Uthibiti wa Airtel, Calvin Simba
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...