Mwanamuziki wa Muziki wa kizazi kipya Maarufu
kama bongo fleva KLEYAH ambaye anakuja kwa kasi katika Tasnia hiyo
hatimaye amezindua nyimbo yake mpya inayokwenda kwa jina la MZOBE MZOBE
wimbo aliomshirikisha msanii maarufu maarufu kutoka THT Barnaba Boy
CLASSIC nyimbo ambayo inatabiriwa kufanya vizuri katika soko la musiki wa
Tanzania.
KLEYAH ambaye ni Mhitimu wa shahada ya mawasiliano kutoka
chuo kikuu cha cha Phoenix nchini marekani na baadae kufanya kazi katika
shirika la kimataifa la UNDP kabla ya kuacha na kuamua kurejea nchini kwa
ajili ya kuendeleza na kukuza sanaa yake Tayari amefanikiwa kufanya kazi na
watayarishaji na wasanii wakubwa ambapo mwaka 2014 alifanikiwa kufanya nyimbo
mbili ambazo zilirekodiwa nchini Kenya na mtayarishaji maarufu nchini
humo Lucas Bikedo pamoja na kufanyia Video kwa watayarishaji maarufu
nchini Kenya kwa sasa OGOPA DJS.
Katika nyimbo yake mpya ambayo ilizinduliwa Tarehe 6 Mwezi
November na kuchezwa katika vituo mbalimbali vya Radio nchini Tanzania na
Africa mashariki kwa ujumla na hatimaye leo umefanyika uzinduzi wa Video yake
ya wimbo wa MSOBE MSOBE unataraji kutambulishwa katika vituo mbalimbali vya
Televission kwa ajili ya kumtambulisha msanii huyo ambaye anaonekana kuja kwa
kasi katika sanaa hii ya music wa kizazi kipya.
Akizungumza nara Baada ya uzinduzi wa Video yake msanii KLEYAH
amesema kuwa kwa sasa mipango yake ni kuendelea kufanya kazi pamoja na
watayarishaji wakubwa nchini Tanzania pamoja na wasanii maarufu ili kukamilisha
album yake ambayo amepanga kuizindua mwezi July mwaka 2016 album ambayo
ametamba kuwa itasheheni aina mbalimbali za misic ili kuwafurahisha mashabiki
wanaofwatilia kazi zake.
Ameongeza aliamua kufanya music kwa kuwa ni kitu ambacho kipo
ndani ya moyo wake huku akieleza kuwa kusoma na baadae kufanya music ni
jambo la kuigwa na wasanii wa Tanzania kwani itamsaidia msanii kutoboa tu si ndani
ya nchi lakini Barani Africa na duniani kwa ujumla
Pia waweza kumfuata kwenye:
Instagram@kleyahmusic
facebook@kleyahmusic
vevo na
utube ni kleyahvevo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...