Na Benedict Liwenga-MAELEZO.

Wanahabari nchini wametakiwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika kuelimisha na kuhamasisha jamii kuhusiana na mabadiliko ya hali ya hewa na afya.

Akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Bi. Neema Rusibamayila wa Wizara hiyo, Dkt. Azma Simba wa Kitengo cha Epidemolojia amesema kuwa suala la kuielimisha jamii lina umuhimu ndo maana kuna haja ya Wizara kushirikiana kwa pamoja katika kutekeleza suala hilo.

Ameeleza kuwa Shughuli za kibinadamu zinachangia kwa kiasi cha asilimia 95 katika kuzalisha na kuongeza kiasi cha gesi joto katika kwenye anga hewa ambapo amezitaja baadhi ya shughuli hizo zikiwemo za uzalishaji viwandani, uzalishaji nishati, kilimo,ufugaji, ukataji miti, uchomaji misitu, usafirishaji, pamoja taka. 

Akitaja athari za mabadiliko ya tabianchi, Dkt. Azma ameeleza kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa joto juu ya wastani, ukame, mafuriko, vimbunga, kubadilika kwa mgawanyo na muda mvua kunyesha pamoja na kuongezeka kwa kina cha bahari.

‘’Sisi sote ni mashahidi wa mabadiliko ya hali hewa yalivyokuwa tishio katika afya ya binadamu. Mabadiliko hayo yameendelea kuleta athari mbalimbali kwa jamii, mazingira na afya ikiwemo upatikanaji wa maji safi na salama, hewa safi, uhakika wa upatikanaji wa chakula na makazi salama’’, alisema Dkt. Azma.

Ameongeza kuwa athari hizo zimepeleke uwepo wa magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambikiza ikiwemo malaria, kuhara, kipindupindu, homa ya bonde la Ufa, denge, utapiamlo, magonjwa ya mfumo wa upumaji na magonjwa ya mfumo wa fahamu.

‘’Jamii ina fursa ya kuboresha afya yake na vizazi vijavyo endapo itaamua kubadilisha mfumo wa maisha unaochangia uzalishaji na ongezeko wa jotogesi unaoharibu (ozone) yaani tabaka hewa’’, aliongeza Dkt. Azma.
 Msimamizi wa Mradi wa Mabadiliko ya Tabia Nchi Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Geofrey Mchau akitoa mada mbele ya Waandishi wa Habari kuhusu mabadiliko ya tabianchi nchini wakati wa Semina Maalum kwa Waandishi hao leo 3 Mei, 2016 Jijini Dar es Salaam. 
 Afisa Habari toka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Bwana Saidi Makola akichangia mada mbele ya Waandishi wa Habari kuhusu mabadiliko ya tabianchi nchini wakati wa Semina Maalum kwa Waandishi hao leo 3 Mei, 2016 Jijini Dar es Salaam.
 Dkt. Azma Simba wa Kitengo cha Epidemolojia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambaye alimwakilisha mgeni rasmi katika ufunguzi wa Semina kwa Waandishi wa Habari kuhusu mabadiliko ya tabianchi akisoma taarifa ya Mkurugenzi toka Wizarani leo 3 Mei, 2016 Jijini Dar es Salaam. 
Afisa Habari toka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Catherine Sungura akichangia mada mbele ya Waandishi wa Habari kuhusu mabadiliko ya tabianchi nchini wakati wa Semina Maalum kwa Waandishi hao leo 3 Mei, 2016 Jijini Dar es Salaam.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...