Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa Uingereza hapa nchini, Mhe. Dianna Melrose alipokuja Wizarani kumuaga mara baada ya kumaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini. Katika mazungumzo yao Waziri Mahiga alimpongeza Balozi Melrose kwa kuiwakilisha nchini yake vema na kuendeleza mahusiano mazuri kati ya Tanzania na Uingereza. Kwa upande wa Balozi Melrose, alisema anaishukuru Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Serikali kwa ujumla kwa ushirikiano aliokuwa anaupata kipindi chote cha uwakilishi wake. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa Canada nchini, Mhe Alexandre Leveque alipokuja Wizarani kumuaga mara baada ya kumaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini. Mhe. Mahiga alimpongeza na kumshukuru kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania katika sekta mbalimbali zikiwemo Elimu na Biashara. Pia Mhe . Alexandre Leveque alitumia fursa hiyo kuishukuru Wizara kwa ushirikiano katika kipindi chake chote cha uwakilishi hapa nchini. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa Ireland nchini, Mhe. Fionnuala Gilsenan alipokuja Wizarani kuaga mara baada ya kumaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini. Mhe. Mahiga alimpongeza na kumshukuru kwa kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Ireland katika sekta mbalimbali. Kwa upande wa Mhe. Gilsenan alitumia fursa hiyo kuishukuru Wizara na Serikali kwa ujumla kwa ushirikiano. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...