SIMU.TV: Msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mutungi, amesema kamati ya baraza la vyama vya siasa nchini litakutana mwishoni mwa mwezi huu kujadili hali ya kisiasa nchini; https://youtu.be/71XK4DcWvBc
SIMU.TV: Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera, imepiga marufuku shughuli zote za uvuvi katika mto kagera mpaka hali ya kiusalama itakapothibitika kutulia;https://youtu.be/wEPexa49Zic
SIMU.TV: Watu wanne wamejeruhiwa baada ya kutokea kwa mapigano kati ya wakulima na wafugaji wilayani Mbalali mkoani Mbeya; https://youtu.be/OFWxKr6lxnI
SIMU.TV: Waziri wa maji na umwagiliaji mhandisi Gerson Lwenge akiwa mkoani Kigoma, amewataka wahandisi wa ngazi za wilaya na mkoa kusimamia kwa umakini miradi ya maji;https://youtu.be/vSTKGVoqa_0
SIMU.TV: Wizara ya kilimo mifugo na uvuvi imefuta mfumo wa utoaji vocha kwa wakulima kupitia mawakala binafsi na badala yake kazi hiyo zimekabidhiwa kampuni za serikali kupitia kamati za ulinzi na usalama; https://youtu.be/KMLWctq_b-g
SIMU.TV: Waziri wa Elimu Prof Joyce Ndalichako, ameitaka tume ya taifa ya sayansi na teknolojia nchini COSTECH kuwa na matumizi mazuri ya pesa za utafiti;https://youtu.be/8-7ssyJaUTY
SIMU.TV: Kikosi cha usalama barabarani kanda maalumu ya Dar Es salaam, kimekusanya fedha zaidi shilingi milioni 161 kutokana na makosa ya barabarani kwa siku za Jumapili na jana Jumatatu; https://youtu.be/1zU5Mfs0tFU
SIMU.TV: Benki ya Afrika imefungua tawi lake wilayani Babati mkoani Manyara ili kuweza kuwafikia wateja wake walioko wilayani humo; https://youtu.be/mwx3gTmFy8U
SIMU.TV: Timu ya Yanga imekamilisha ratiba ya michuano barani Afrika kwa kipigo cha magoli 3-1 katika mchezo wake dhidi ya TP Mazembe uliopigwa leo jijini Lubumbashi;https://youtu.be/d38dUiow2c8
SIMU.TV: Timu ya Taifa ya vijana Serengeti boys inatarajia kuweka kambi yake nje ya nchi kuweza kujiandaa kikamilifu na mchezo wake kati ya Congo au Namibia;https://youtu.be/utySjyQEHEQ
SIMU.TV: Timu ya African Lyon imesema bado inaendelea vizuri na mazoezi kwa ajili ya kujiweka sawa na michezo yake inayofuata baada ya kutoka sare katika mchezo wake wa kwanza dhidi ya Azam Fc; https://youtu.be/lSpY8aHQEyE
SIMU.TV: Baadhi ya wajasiliamali wadogo kutoka mikoa ya kanda ya ziwa wameanza kutengeneza mipira ya miguu baada ya kupewa mafunzo na taasisi ya teknolojia kampasi ya Mwanza; https://youtu.be/3BlEBwIa3Ng
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...