Moja ya kadi za kieletroniki.
Mashabiki wa Mpira wakiwa wamepanga foleni ya kwenda kukata tiketi za kieletroniki jijini Dar es Salaam leo.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
MFUMO mpya wa kadi za kieletroniki umeonekana kupokelewa kwa mwitikio mkubwa sana na wananchi wengi kujitokeza kupata kadi zitakazowawezesha kukata tiketi kwa njia ya kuingia uwanjani kuangalia mpira.

Katika maeneo mbalimbali kadi hizo zimekuwa zikitolewa kwa shilingi 1000 hadi 3000 zimekuwa chachu ya serikali kupata mapato halisi tofauti na ulivyokuwa mfumo wa tiketi za kawaida na utatakiwa kuisajili kwa jina lako la kwenye kitambulisho cha kupigia kura sambamba na namba ya simu unayoitumia na utatakiwa kujaza fedha na kulipia kulingana na sehemu unayotaka kwenda kukaa.

Mfumo huo rasmi unaanza kutumika Oktoba 01 kwenye mchezo baina ya Yanga na Simba na utamlazimu mwananchi au shabiki anayetaka kushuhudia mchezo huo kuwa na kadi maalumu atakayotumia kuingilia mlangoni na kumuonyesha ni mahala gani anatakiwa kwenda kukaa

Kuja kwa mfumo huo timu mbalimbali zitaacha kulalamika kuhusiana na tiketi feki zilizokuwa zinauzwa na watu wasiojulikana na kuhujumu mapato ya timu zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...