NA K-VIS BLOG, MTWARA

SHIRIKA la Umeme nchini (Tanesco), limefanikiwa kukarabati mashine namba 6 iliyokuwa imeharibika na kuiwasha kwa ajili ya kutoa huduma ya umeme kwa mikoa ya Lindi na Mtwara.

Hatua ya kuwashwa kwa mtambo huo ni juhudi za shirika hilo za kuimarisha hali ya upatikanaji umeme kwa wananchi kusini huku ikiwa ni siku moja baada ya Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani alipotembelea Kituo cha kufua umeme kwa gesi .

Akizungumza leo mjini hapa, Kaimu Mkurugenzi wa Tanesco, Mhandisi Dk. Tito Mwinuka ambaye amepiga kambi mkoani humo pamoja na watalaamu wengine, alisema kuwa mitambo iliyokuwa ikifanya kazi ilikuwa minne lakini baada ya juhudi kubwa za wataalamu wa Tanesco hadi kufikia jana jioni wamefanikiwa kuwasha mashine hizo zenye uwezo wa kuzalisha Megawati 16.
Mafundi wakiratibu zoezi la ukarabati wa mshine .
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Tito Mwinuka, (wakwanza kushoto), na viongozi wengine wa Shirika hilo, wakifuatilia maendeleo ya ukarabati wa mitambo ya kufua umeme mkoani Mtwara leo Oktoba 17, 2017.
Mafundi wa TANESCO wakiendelea na ukarabati wa mshine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...