Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Taifa la Madini (Stamico),Zena Kangoyi akizungumza na waandishi wa habari juu mafanikio ya stamico baada ya maboresho yaliyofanywa katika shirika hilo katika Ofisi Makao Makuu jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Mkurugenzi wa  Utafiti  na Uchorongaji ,Alex Rutagwelela akizungumza na waandishi wa habari juu Stamico linavyosimamia majukumu yake katika katika kuendeleza wachuimbaji wadogo iliyofanyika leo Makao Makuu ya Stamico,jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala,Beatrice akizungumza na waandishi wa habari juu Stamico linavyoweza kusimamia miradi yake na uwezo wa Shirika hili iliyofanyika leo Makao Makuu ya Stamico jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Stamico,Zena Kangoyi akiwa na baadhi ya wakurugenzi wakati akieleza mafanikio ya shirika hilo kwa waandishi wa habari iliyofanyika Makao Makuu jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
SHIRIKA la Taifa la Madini (Stamico)limesema kuwa kutokana na kuwepo kwa maboresho katika shirika hilo limezidi kujitanua katika utoaji wa utaalam kwa wachimbaji wadogo jinsi ya kuchimba madini kisasa na kuachana uchimbaji duni.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Kaimu Mkurugenzi Mtendaji,Zena Kongoyi amesema kuwa shirika licha ya kuweka miradi ya kusaidia wachimbaji wadogo lakini wameweza kuwekeza uchimbaji wa madini kwa kushirikiana na kampuni zingine kutokana sharia ziliwekwa baada ya mabaoresho ya shirika hilo.

Amesema baadhi ya miradi ya uzalishaji wa madini imeanza kuzalisha na kuweza shirika kutoka hatua moja  kwenda nyingine katika katika utaoji huduma pamoja kukuza uchumi wa nchi pamoja kuongeza ajira nchini kutokana na miradi ya uzalishaji wa dhahabu.

Zena amesema kuwa shirika limeanzisha miradi kuendeleza wachimbaji wadogo kitaalamu na ufundi kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati na Madini pamoja na Mradi wa Usimamizi Endelevu (SMMRP) katika kuwaondoa katika uduni.

Amesema katika mradi wa Stamigold umesafirisha na kuuza dhahabu katika nchi ya Switzerland kwa kiasi cha Wakia 12,923.35 na kuingizia shirika la Taifa la Madini (Stamico)na taifa kwa ujumla Dola za Kimarekani Milioni 15.6. na kuaza kurejesha mrabaha wa asilimia 4.0 ya mauzo sawa n ash.1.3 za serikali na Wizara ya Nishati na Madini na kulipa ushuru sh.milioni 40..

Aidha amesema shirika limeweza kuanzisha mradi wa ununuzi wa madini ghafi ya bati kutoka kwa wachimbaji wadogo wa maeneo ya vijiji vya Kabingo,Murongo ,Syndicate na Rugasha katika Wilaya Kyerw,mkoani Kagera  na kuyauza madini hayo kwenye soko la nje ya nchi ikiwa na lengo la kuwasaidia wachimbaji wadogo .




Zena amesema wako katika mazungumzo na Benki ya TIB kuweza kukopa Dola za Kimarekani 700,00090000  kwa ajili ya kununua mitambo hali ambayo shirika litaweza kukua katika kuendesha miradi mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...